Azam FC inatarajia kumualika AL Hilal ya Ibenge kwenye mchezo wao wa kirafiki Chamazi Complex huku mechi ya kwanza timu hiyo kutoka Sudan ikitoa sare ya kufungana 1-1 dhidi ya Namungo FC.

Mchezo huo unatarajiwa kupigwa majira ya saa 1:00 usiku huku Al Hilal wakijiandaa na michuano ya Klabu Bingwa Barani Afrika yanayotarajiwa kuanza mwezi ujao na wataanza dhidi ya Mamelod Sundowns mechi ya kwanza.
Azam FC wao wametoka kupoteza mechi yao ya mwisho ya Ligi sasa na matumaini ya ubingwa yamepotea kutokana na kupitwa pointi nyingi na anayeongoza Ligi Yanga ambae kapoteza mchezo mmoja pekee.

Al Hilal kwenye Ligi yao huko Sudan wapo nafasi ya kwanza huku wakiwa na pointi zao 44 baada ya kucheza michezo 17, wakiwa wameshinda michezo yao 14, sare mbili na kupoteza mchezo mmoja.

