Mudathir Yahya kiungo wa Yanga ubora wake uleule unaendelea msimu wa 2024/25 kwa mujibu wa Maulid Kitenge ameweka wazi kuwa kwa Muda simu zitaita sana.

Agosti 4 katika utambulisho wa wachezaji wapya na wale waliokuwa na kikosi cha Yanga msimu wa 2023/24 kwenye kilele cha Wiki ya Mwananchi wakati ubao wa Uwanja wa Mkapa ukisoma Yanga 2-1 Red Arrows alipachika bao moja.
Dakika ya 64 Mudathir aliweka usawa bao la Red Arrows ambalo lilifungwa kipindi cha kwanza kupitia kwa Ricky Banda dakika ya 5 kwa mabingwa wa Kagame Cup.
Bao la pili la ushindi kwa Yanga lilifungwa na Aziz Ki dakika ya 90 kwa pigo la penalti baada ya beki wa Red Arrows kumchezea faulo Nickson Kibabage


