Kocha wa Real Madrid Carlo Ancelotti anatarajiwa kuondoka kwenye klabu hiyo mwishoni mwa msimu huu.
Carlo Ancelotti alirejea kwenye kikosi cha Real kwa mara ya pili na anatarajiwa kuachana na timu hiyo mwishoni mwa msimu huu huku akitajwa kuwa anaweza kuchukua timu ya Taifa ya Brazil.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa.
Mkataba wa Ancelotti na timu hiyo ya Bernabeu itamalizika mwishoni mwa mwakani, lakini inaelezwa kuwa makubaliano ya pande zote mbili yameshafikiwa na kocha huyo mwenye mafanikio makubwa ataondoka baada ya michezo mitano ijayo.
Madrid ilichapwa mabao 3-2 juzi na Barcelona kwenye fainali ya Copa del Rey lakini pia ikiwa imeshatupwa nje kwenye michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya ilipotolewa na Arsenal mwanzoni mwa mwezi huu.
Kwa sasa timu hiyo ipo pointi nne nyuma ya Barcelona kwenye msimamo wa La Liga huku kukiwa na michezo mitano ambayo ndiyo inaweza kuwa muhimu zaidi kwa timu hiyo kwani haina uhakika wa kombe lolote msimu huu.
Vyanzo vinasema kuwa kocha huyo anatakiwa na timu ya Taifa ya Brazil na ataanza kazi yake mwishoni mwa msimu huu akiwa anatakiwa kuhakikisha timu hiyo inafanya vizuri kwenye fainali zijazo za Kombe la Dunia.