Chelsea Yamtimua Graham Potter

Klabu ya Chelsea imemtimua Graham Potter baada ya kuwa mkufunzi mbaya asiyepata matokeo ambayo timu hiyo ikihitaji.

 

Chelsea Yamtimua Graham Potter

Potter mwenye miaka 47, aliondoka Brighton na kuchukua mikoba ya Stamford Bridge Septemba mwaka jana baada ya kuondoka kwa kocha aliyeshinda Champions League Thomas Tuchel.

Hata hivyo kocha huyo wa zamani wa Seagulls alishindwa kupata matokeo bora kutoka kwa kikosi cha nyota alichorithi, huku usajili wa Januari ukionekana kumuongezea matatizo.

Na Chelsea wamethibitisha kwamba Bruno Saltor atachukua mikoba ya kocha mkuu kwa muda kufuatia kichapo cha 2-0 Jumamosi dhidi ya Aston Villa, ambacho kilipelekea timu ya Potter kuporomoka hadi 10 la pili kwenye msimamo wa EPL.

Chelsea Yamtimua Graham Potter

Wamiliki wa pamoja Todd Boehly na Behdad Eghbali walisema: “Kwa niaba ya kila mtu kwenye klabu, tunataka kumshukuru Graham kwa dhati kwa mchango wake. Tuna heshima ya juu zaidi kwa Graham kama kocha. Daima amekuwa akijiendesha kwa weledi na uadilifu na sote tumesikitishwa na matokeo haya.”

Pamoja na mashabiki wetu wa ajabu, sote tutakuwa nyuma ya Bruno na timu tunapozingatia msimu uliobaki. Tumebakiza mechi 10 za Ligi Kuu na robo fainali ya Ligi ya Mabingwa mbele. Tutaweka juhudi na kujitolea katika kila moja ya mechi hizo ili tuweze kumaliza msimu kwa kasi. Taarifa hiyo ilisema.

Potter, ambaye alitatizwa na majeraha kwa wachezaji kama N’Golo Kante na Reece James, aliendelea kusakata kabumbu na kubadilisha safu yake ya kuanzia alipojaribu kutafuta wachezaji wake bora zaidi na kulazimisha falsafa yake.

Chelsea Yamtimua Graham Potter

Lakini Boehly na Co waliamua inatosha baada ya mchezo dhaifu dhidi ya Villa kuwaacha Chelsea wakiwa nafasi ya 11 kwenye ligi.

Chelsea watawakaribisha Liverpool kesho usiku kabla ya kumenyana na Wolves Jumamosi.

Acha ujumbe