Mbappe Ajikita Kikamilifu PSG Licha ya Huzuni ya Kombe la Dunia

Kylian Mbappe hakuweza kukubali kushindwa kwa Ufaransa katika fainali ya Kombe la Dunia na Argentina hivi karibuni, lakini mshambuliaji huyo anasema sasa anajikita kabisa Paris Saint-Germain.

 

Mbappe Ajikita Kikamilifu PSG Licha ya Huzuni ya Kombe la Dunia

Licha ya kufunga mabao matatu ‘hat-trick’ kwa upande wa Didier Deschamps kwenye fainali, Mbappe na wachezaji wenzake wa Kimataifa walikosa nafasi wakati Les Bleus walipochapwa kwa mikwaju ya penalti katika mchezo wa fainali wa Qatar 2022.

Wakati mchezaji mwenzake Lionel Messi bado hajarejea Paris kufuatia ushindi wake, Mbappe alirejea haraka kwenye uwanja wa nyumbani, na kupata ushindi wa 2-1 dhidi ya Strasbourg kwenye Ligue 1 jana licha ya Neymar kutolewa nje kwa kadi nyekundu baada ya saa moja tu.

Akizungumza baada ya kufunga penalti dakika ya 96 aliyojishindia mwenyewe, mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 24 alikiri machungu ya kupoteza kwa Ufaransa huko Doha yatakaa naye milele, lakini alisisitiza kuwa haoni wachezaji wenzake wanapaswa kulipa gharama ya hisia hizo.

Mbappe Ajikita Kikamilifu PSG Licha ya Huzuni ya Kombe la Dunia

Mbappe amesema kuwa; “Binafsi, sitawahi kukataa, lakini klabu yangu haiwajibiki kwa kushindwa huku na timu ya Taifa. Ninajaribu kurejea na nguvu chanya, nilijaribu kuleta nguvu kwa timu yangu na tunatumai kuendeleza msimu wetu bila kupoteza. Ilikuwa Kombe la Dunia, Klabu haina uhusiano wowote nayo.”

Aliporejea PSG kwa haraka kutoka kwenye majukumu ya Kimataifa, Mbappe alisisitiza dhamira yake ya kuweka mambo ya klabu na nchi tofauti, na kuongeza: “Ujumbe ni rahisi. Inaonyesha kwamba haijalishi nini kitatokea kwa timu ya taifa, PSG ni kitu kingine. Bado nimedhamiria kurudisha mataji yote katika mji mkuu.”

Bao la dakika za lala salama la Mbappe dhidi ya Strasbourg linamaanisha kuwa kikosi hicho cha Christophe Galtier kimepoteza pointi mara mbili pekee kwenye Ligue 1 msimu huu, na rekodi ya kutoshindwa Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya pia.

Mbappe Ajikita Kikamilifu PSG Licha ya Huzuni ya Kombe la Dunia

Mchezo unaofuata watacheza dhidi ya Lens ambao wapo nafasi ya pili katika Siku ya Mwaka Mpya, ambapo wanatarajia kufunguka zaidi mchana kati yao na mpinzani wao mkuu, ambao wana pointi nane mbele ya kuwa wamecheza mchezo mmoja zaidi.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.