Allegri: "Ni Muhimu Kufikisha Pointi 50, Lakini Milan Wanapaswa Kufanya Vizuri Zaidi.”

Massimiliano Allegri anaamini bado kuna nafasi ya kuboresha kwa kikosi chake cha Milan, licha ya kupata ushindi wa mabao 3-0 ugenini dhidi ya Bologna bila ya Rafael Leao, Christian Pulisic na Alexis Saelemaekers usiku wa jana.

Allegri: "Ni Muhimu Kufikisha Pointi 50, Lakini Milan Wanapaswa Kufanya Vizuri Zaidi.”

Rossoneri waliendeleza rekodi yao ya kutopoteza katika Serie A hadi kufikia mechi 22 mfululizo, shukrani kwa mabao ya Ruben Loftus-Cheek, Christopher Nkunku na Adrien Rabiot katika ushindi huo wa 3-0 uliopatikana kwenye Uwanja wa Dall’Ara jana.

Akizungumza na DAZN baada ya mechi, Allegri alieleza kuwa Milan walicheza vizuri kwa sababu waliweza kunufaika na ushirikiano wa washambuliaji Nkunku na Loftus-Cheek, ambao hawakuwa wamewahi kuanza pamoja safu ya ushambuliaji kabla ya mechi ya jana.

“Nkunku na Loftus-Cheek ni wachezaji wenye ubora mkubwa sana. Ilikuwa lazima tuchukulie mechi hii kwa umakini, kwa sababu Bologna wana safu nzuri ya ulinzi. Ni timu hatari inayocheza vizuri. Wachezaji walifanya vizuri katika ulinzi na pia kwenye mashambulizi.” Alisema Allegri

Allegri: "Ni Muhimu Kufikisha Pointi 50, Lakini Milan Wanapaswa Kufanya Vizuri Zaidi.”

Licha ya ushindi huo, Allegri anaamini bado kuna mambo ya kuboresha katika kikosi cha sasa cha Milan.

Kocha huyo aliendelea kusema kuwa ilikuwa mechi nzuri usiku wa jana. Wanapaswa kuboresha zaidi katika umiliki na matumizi ya mpira. Walicheza vizuri kwa sababu Nkunku na Loftus-Cheek walifanya vizuri, wakiwasaidia kucheza kwa utulivu na kuongeza nguvu kwenye mashambulizi.

Alipoulizwa ni sehemu gani ya mchezo aliyofurahishwa nayo zaidi, Ilikuwa muhimu kufikisha pointi 50 msimu huu kwa sababu lengo letu limekuwa kufika katika nafasi nne za juu. Allegri alisema

Tulilinda vizuri baada ya kuongoza 3-0, kutoruhusu bao ni jambo zuri kila wakati. Ni muhimu zaidi kuangalia yaliyo mbele, kwa sababu msimu bado ni mrefu na tunahitaji pointi nyingi zaidi ili kufuzu Ligi ya Mabingwa Ulaya. Tutafurahia mapumziko haya kwa sababu hatuchezi Jumapili, na tunatarajia kuwa na wachezaji wetu wote tayari tena. Alimaliza hivyo.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.