Mbappe Aendeleza Rekodi Kombe la Dunia

Nyota wa timu ya Taifa ya Ufaransa Kylian Mbappe ndiye mfungaji bora wa Kombe la Dunia mpaka sasa akiwa amefunga mabao matano na kuongeza mabao manne aliyofunga kwenye kampeni ya Ufaransa ya ushindi wa Kombe la Dunia 2018.

 

Mbappe Aendeleza Rekodi Kombe la Dunia

Akiwa tayari amempita Diego Maradona wa Argentina, aliyefunga nane, huku Mreno Cristiano Ronaldo pia akifikisha idadi hiyo. Mbappe ambaye ana umri wa miaka 23, ndiye mchezaji mwenye umri mdogo zaidi kupachika mabao Kombe la Dunia.

Mbappe amefumania nyavu mara tisa, toka 2018 mpaka sasa akivunja rekodi iliyokuwa ikishikiliwa na Eusebia wa Ureno aliyetupia nyavuni mara 8 akiwa na miaka 24 na siku 182.

Mbappe Aendeleza Rekodi Kombe la Dunia

Mchezaji huyo alieisadia Ufaransa kubeba Kombe hilo kwenye kikosi cha Deschamps ni mshambuliaji muhimu sana kutokana na ubora ambao anao hadi sasa kwani licha ya kuwa na uwezo mkubwa wa kupachika mabao anatoa pasi za mabao.

Ufaransa wanatarajia kuvaana na Uingereza katika hatua ya robo fainali ya michuano hii siku ya Jumamosi huku macho mengi ya watu wakiisubiria mechi hii kuona Mabingwa watetezi watafanya nini mwaka huu mbele ya vijana wa Southgate.

Mbappe Aendeleza Rekodi Kombe la Dunia

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.