Juventus Wakutana na Sassuolo Kujadili Kuhusu Frattesi Anayelengwa na Inter

Gianluca Di Marzio anaripoti kuwa kaimu mkurugenzi wa michezo wa Juventus Giovanni Manna kwa sasa anakutana na rais wa Sassuolo Giovanni Carnevali kujadili kuhusu dili la Davide Frattesi.

 

Juventus Wakutana na Sassuolo Kujadili Kuhusu Frattesi Anayelengwa na Inter

Kiungo huyo mwenye umri wa miaka 23 anaonekana kupangwa kuondoka Reggio-Emilia msimu huu wa joto baada ya miaka michache ya kuvutia, huku pande nyingi za juu za Italia zikipigania kuinasa saini yake.

Roma na Juventus kwa muda mrefu wamekuwa wakivutiwa na Frattesi, na katika wiki za hivi karibuni Inter wamejitokeza kujaribu kumnasa Muitaliano huyo, ambaye wanaamini angeunda ushirikiano wa kutisha na Nicolo Barella.

Di Marzio anaelezea jinsi Manna na Carnevali kwa sasa wako kwenye mkutano wa kujadili vigezo vya mkataba wa Frattesi, huku Juventus wakitarajia kumjumuisha Koni De Winter katika dili la nyota huyo wa Sassuolo.

Juventus Wakutana na Sassuolo Kujadili Kuhusu Frattesi Anayelengwa na Inter

La Gazzetta dello Sport hivi majuzi ilipendekeza kuwa Inter walikuwa wamekubali masharti ya mkataba na Sassuolo, wakiwa tayari kulipa €30m pamoja na Samuele Mulattieri kwa ajili ya kiungo huyo wa Kiitaliano, lakini Juventus wanakataa kukata tamaa.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.