Gianluca Di Marzio anaripoti kuwa kaimu mkurugenzi wa michezo wa Juventus Giovanni Manna kwa sasa anakutana na rais wa Sassuolo Giovanni Carnevali kujadili kuhusu dili la Davide Frattesi.

Kiungo huyo mwenye umri wa miaka 23 anaonekana kupangwa kuondoka Reggio-Emilia msimu huu wa joto baada ya miaka michache ya kuvutia, huku pande nyingi za juu za Italia zikipigania kuinasa saini yake.
Roma na Juventus kwa muda mrefu wamekuwa wakivutiwa na Frattesi, na katika wiki za hivi karibuni Inter wamejitokeza kujaribu kumnasa Muitaliano huyo, ambaye wanaamini angeunda ushirikiano wa kutisha na Nicolo Barella.
Di Marzio anaelezea jinsi Manna na Carnevali kwa sasa wako kwenye mkutano wa kujadili vigezo vya mkataba wa Frattesi, huku Juventus wakitarajia kumjumuisha Koni De Winter katika dili la nyota huyo wa Sassuolo.

La Gazzetta dello Sport hivi majuzi ilipendekeza kuwa Inter walikuwa wamekubali masharti ya mkataba na Sassuolo, wakiwa tayari kulipa €30m pamoja na Samuele Mulattieri kwa ajili ya kiungo huyo wa Kiitaliano, lakini Juventus wanakataa kukata tamaa.

