Ahmed Arajiga ametangazwa kuwa mwamuzi wa kati wa mchezo wa Ligi Kuu Bara unaotarajiwa kuchezwa Uwanja wa Mkapa, Machi 8 2025 ambapo wababe wawili wanatarajiwa kukutana Yanga na Simba.

Ikumbukwe kwamba Arajiga alikuwa mwamuzi kwenye mchezo wa Mzizima Dabi uliochezwa Uwanja wa Mkapa baada ya dakika 90 ubao ulisoma Simba 2-2 Azam FC wababe hao walipogawana pointi mojamoja baada ya mchezo kukamilika.
Ikumbukwe kwamba kwenye mchezo wa mzunguko wa kwanza ni Ramadhan Kayoko alikuwa ni mwamuzi wa kati ila mzunguko wa pili jina lake halipo kwenye orodha ya waamuzi. Katika mchezo huo baada ya dakika 90 ubao wa Uwanja wa Mkapa ulisoma Simba 0-1 Yanga, bao la Kelvin Kijili aliyejifunga lilidumu mpaka mwisho wa mchezo.
Pia meridianbet inatoa michezo ya kasino ya mtandaoni kama vile, Aviator, poker, Roullette, sloti na mingine kibao. Ingia meridianbet na ucheze sasa.



