PSG wamethibitisha kumsajili Ousmane Dembele kwa mkataba wa miaka mitano kutoka Barcelona, ambaye alisema ada hiyo ilikuwa euro milioni 50.4.
Tangu kuwasili kwake kutoka Borussia Dortmund mwaka 2017 kwa ada iliyoripotiwa kuwa ya hadi £135.5m, Dembele alicheza mechi 185 na kufunga mabao 40 kwa wababe hao wa LaLiga.
Odds kubwa kasino ya mtandaoni na michezo ya sloti ni vitu vinavyoweza kubadilisha maisha yako kwa kukupatia pesa nyingi. Ingia mchezoni hapa.
Wakati Dembele akiwa Barcelona pia alishinda mataji matatu ya ligi ya Uhispania, Vikombe viwili vya Uhispania na Supercups mbili za Uhispania.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26 ameichezea Ufaransa mara 37 na kushiriki Kombe la Dunia mwaka jana nchini Qatar, ambapo Les Bleus walimaliza kama washindi wa pili.
Aviator, poker, Roullette, Wild Icy Fruits, Piggy Party na mingine kibao upige pesa na Meridianbet. Ingia www. meridianbet.co.tz.
Dembele aliiambia tovuti ya klabu: “Nina furaha kujiunga na PSG na siwezi kusubiri kuichezea klabu yangu mpya. Natumai naweza kuendelea kukua hapa na kuwafanya mashabiki wote wa klabu hiyo wajivunie.”