Milan wako tayari kutangaza kumsajili Christian Pulisic kutoka Chelsea na mchezaji huyo wa kimataifa wa USMNT atavaa jezi nambari 11 huko San Siro.

Pulisic alifanyiwa uchunguzi wa kimatibabu na Milan jana kabla ya kusaini mkataba wake na Rossoneri.
Picha kutoka Casa Milan zinaonyesha jezi ya Pulisic tayari inauzwa na nambari 11 nyuma yake. Gazeti la Tuttosport limethibitisha kuwa winga huyo wa Marekani atavaa Nambari ya awali ya gwiji wa klabu Zlatan Ibrahimovic.
Chaguo jingine lilikuwa namba 22, ambalo lilikuwa likivaliwa na nguli mwingine wa klabu hapo awali, Ricardo Kaka.

Milan wanatarajiwa kuthibitisha saini ya Pulisic siku ya leo na kuthibitisha rasmi jezi yake namba 2023-2024. Atahamia San Siro kutoka Chelsea kwa mkataba wa thamani ya zaidi ya €20m.
Nahodha huyo wa USMNT alifunga mabao 26 katika mechi 145 akiwa na Chelsea, ambapo aliwasili mwaka 2019.
Ni mchezaji wa nne kusajiliwa na Milan majira ya kiangazi baada ya Ruben Loftus-Cheek, Luka Romero na Marco Sportiello.

