Mshambuliaji wa Chelsea, Raheem Sterling anafurahia sasa kurejea kwenye ubora wake wa soka baada ya mechi ya jana usiku dhidi ya Luton.
Sterling alifunga bao la kufutia machozi dhidi ya Hatters kwenye Uwanja wa Stamford Bridge dakika ya 17 kabla ya kuongeza bao hilo muda mfupi baada ya dakika ya lala salama.
Odds kubwa kasino ya mtandaoni na michezo ya sloti ni vitu vinavyoweza kubadilisha maisha yako kwa kukupatia pesa nyingi. Ingia mchezoni hapa.
Mshambuliaji mwenzake Nicolas Jackson alikamilisha ushindi wa 3-0 wa kwanza wa umiliki wa Mauricio Pochettino na Sterling sasa anataka kuona maboresho zaidi katika msimu wake wa pili na The Blues.
Mchezaji huyo wa kimataifa wa Uingereza mwenye umri wa miaka 28 aliambia tovuti rasmi ya klabu: “Mengi yametokea katika maisha yangu ya soka. Nimekuwa na changamoto mpya ambayo imekuwa ngumu na kichwa chako kinaweza kuwa na ukungu. Mapenzi yangu kwa mpira wa miguu ni mengi na mimi ni mdogo sana katika umri wa miaka 28 kuruhusu maisha yangu ya soka yatimie.
Beti na Meridianbet kwa odds kubwa na machaguo kibao, pia unaweza kubashiri mubashara
Sterling amesema kuwa anahitaji kudumisha viwango ambavyo amejiwekea miaka michache iliyopita na kuendelea. Alikuja na visingizo lakini kwasasa hiyo hamna. Anataka kureja bora zaidi na hakuna kingine.
Pochettino alimsifu Sterling kwa mchango wake katika ushindi huo, ambao uliifanya Chelsea kupanda hadi nafasi ya nane kwenye msimamo wa ligi kwa pointi nne kufuatia sare ya nyumbani na Liverpool na kushindwa Jumapili iliyopita na West Ham.
Kocha huyo wa Argentina alisema: “Nadhani anastahili sifa kamili kwa uchezaji wake. Ana ubora na anaweza kuipatia timu mabao na asisti. Nimefurahishwa sana naye. Aliniambia ulikuwa msimu mgumu kwake msimu uliopita. Utendaji wake wa kazi ni wa kushangaza halafu ana kasi, kukimbia nyuma ya safu ya ulinzi na kisha ubora kwenye miguu.”
Aviator, poker, Roullette, Wild Icy Fruits, Piggy Party na mingine kibao upige pesa na Meridianbet. Ingia www. meridianbet.co.tz.
Ni suala la muda tu kwamba atafunga mabao pia. Anashangaza. Ni vigumu kupata mchezaji kama yeye sokoni. Kwangu, atakuwa mmoja wa washambuliaji wakubwa. Ana uwezo wa kuwa. Alisema Pochettino.
Vijana wa Pochettino watacheza tena Jumatano, watakapoikaribisha AFC Wimbledon katika raundi ya pili ya Kombe la EFL.