Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) itashuka dimbani hii leo kumenyana dhidi ya Uganda kwenye michuano ya kuwania kufuzu Afcon huku mechi hiyo ikitarajiwa kupiga majira ya saa 10:00 jioni.

Taifa Stars wamefanya mazoezi hapo jana katika dimba la Suez Canal kwaajili ya kujiweka fiti kwenye mchezo huu wa leo huku wakiahidiwa ahadi ya Milioni 500 endapo watafanikiwa kufuzu kucheza Afcon.
Wachezaji wote wapo fiti kwaajili ya huu mchezo wa leo baada ya mazoezi ambayo wameyafanya huku nahodha wa timu hiyo ya Taifa Mbwana Samatta akisema kuwa wamejiandaa vizuri kuwakabili Uganda.

Uganda amekuwa msumbufu sana anapokutana na Tanzania kwani mechi ya mwisho kukutana ilikuwa ya kirafiki na Taifa Stars alipoteza mchezo huo. Sasa wanakutana kwenye mechi muhimu ambayo kila timu inahitaji matokeo. Je nani kuondoka mbabe?

