Klabu ya Liverpool ambayo ipo chini ya kocha mkuu Jurgen Klopp amepata ushindi wake wa ugenini msimu huu hapo jana baada ya kumbamiza Tottenham Hot Spurs kwa mabao 2-1 akiwa ugenini.

Mchezo huo ulipigwa majira ya saa 19:30, huku kipindi cha kwanza kabisa Liverpool wakajipatia mabao 2 ya kuongoza kupitia kwa mchezaji wao Mohamed Salah katika dakika ya 11 na 40.
Waliporudi kutoka kipindi cha pili vijana wa Antonio Conte walibadilika na kuanza kushambulia lango la mpinzani wake na mpaka kufikia dakika ya 70 mshambuliaji wao Harry Kane akaifungia timu yake bao la kwanza lakini halikutosha.

Spurs walijaribu kupiga mashuti 5 yaliyolenga lango na kwa upande wa majogoo wao walipiga mashuti 6 huku umiliki wa mpira ukiwa haujatofautiana kwa kiwango kikubwa na timu zote zikionekana kuhitaji ushindi huo wa jana.
Ushindi huo wa Liverpool unamsogeza hadi nafasi ya 8 wakati Spurs akiwa nafasi ya 4, mchezo ujao wa Majogoo itakuwa ni dhidi ya Derby Country kwenye michuano ya Carabao Cup kabla ya kuja kucheza dhidi ya Southampton.

Wakati kwa Conte yeye atakipiga dhidi ya Nottingham Forest kwenye michuano hiyo na baadae kwenye ligi kumkaribisha Leeds kwenye ligi.

Ulishawahi kuwaza kuwa rubani wa maisha yako!! Kuwa rubani wa mchezo pendwa wa Aviator wa kasino mtandaoni. Aviator bonanza inazidi kutoa michongo ya mkwanja kwenye nyumba ya mabingwa. Unarusha ndege yako na unashinda, kuwa rubani wa kujivunia kwa kuibuka na mkwanja leo.
BONYEZA HAPA

