Klabu ya Liverpool leo itashuka dimbani kumenyana na klabu ya Tottenham Hotspurs itakayokua nyumbani katika dimba lao la Tottenham Hotspur, Vijogoo watakua wanajitafuta kwenye ligi kuu ya Uingereza baada ya kua na mfululizo wa matokeo mabaya.
Klabu ya Liverpool imekua kwenye wakati mgumu msimu huu kwenye ligi kuu ya Uingereza baada ya kushinda michezo minne tu kwenye ligi kuu ya Uingereza kati ya michezo 12 ambayo wamecheza mpaka sasa.
Vijogoo hao wa Anfield leo wanaenda kucheza na Tottenham huku wakitoka kuvunja rekodi ya Napoli ya kutokufungwa kwenye michuano yote kwenye mchezo wa ligi ya mabingwa ulaya na kupata ushindi wa bao mbili kwa bila.
Vijana wa Jurgen Klopp leo wataenda kutafuta ushindi wa tano kwenye ligi hiyo huku wakiamini inaweza kua mechi ya kurudisha hali ya kujiamini kwa timu hiyo baada ya kutoka kupoteza dhidi ya Leeds nyumbani wiki iliyopita.
Klabu ya Tottenham nao watakua wanahakikisha wanapata ushindi dhidi ya Liverpool kwani nao wanahitaji kuendelea kubaki ndani ya nne bora kwenye msimamo wa ligi hiyo.

Ulishawahi kuwaza kuwa rubani wa maisha yako!! Kuwa rubani wa mchezo pendwa wa Aviator wa kasino mtandaoni. Aviator bonanza inazidi kutoa michongo ya mkwanja kwenye nyumba ya mabingwa. Unarusha ndege yako na unashinda, kuwa rubani wa kujivunia kwa kuibuka na mkwanja leo.
BONYEZA HAPA

