Tuchel Anaona Wigo Mpana wa Kuiboresha Bayern Licha Ushindi Mwepesi wa Klassiker

Mechi ya kwanza ya Thomas Tuchel kama kocha wa Bayern Munich inaweza kuwa ushindi mzuri kwake dhidi ya wapinzani wao Borussia Dortmund, lakini anajua kuna kazi kubwa ya kufanya.

 

Tuchel Anaona Wigo Mpana wa Kuiboresha Bayern Licha Ushindi Mwepesi wa Klassiker

Tuchel alichukua nafasi ya Julian Nagelsmann wakati wa mapumziko ya kimataifa, na mchezo wake wa kwanza dimbani ulikuwa ni Klassiker wa jana dhidi ya klabu yake ya zamani Dortmund, ambao walikuwa wameshinda mechi tisa kati ya 10 za kwanza za ligi mwaka wa 2023 na kuwaacha kileleni mwa Bundesliga.

Lakini Bayern waliwapita hadi kileleni kwa kuwafunga hapo jana ambapo hadi sasa tofauti ya pointi kati yao ni mbili pekee.

Makosa ya Gregor Kobel na bao mbili la Thomas Muller yaliwafanya mabingwa hao watetezi mara 10 kuwa mbele kwa mabao 3-0 ndani ya dakika 23.

Tuchel Anaona Wigo Mpana wa Kuiboresha Bayern Licha Ushindi Mwepesi wa Klassiker

Kingsley Coman walifanya mambo kuwa 4-0 muda mfupi baada ya kipindi cha kwanza kwenda mapumziko, na ingawa mabao ya kujifariji kutoka kwa Emre Can na Donyell Malen yalizidisha ushindi wao, Bayern sasa wanaonekana kuwa na nafasi nzuri ya kutwaa ubingwa wa 11 mfululizo wa Bundesliga.

Licha ya mwanzo mzuri wa uongozi wake, Tuchel anasisitiza bado kuna kazi kubwa ya kufanya ikiwa Bayern wanataka kufika pale anapotaka, akiiambia Sky TV: “Nilikuwa na wasiwasi sana leo. Ilikuwa hatua nzuri ya kwanza lakini bado kuna nafasi kubwa ya kuboresha na ilikuwa ni jambo la kipumbavu sana, tulitaka kuwa na utawala zaidi. Tulianza kwa wasiwasi sana mchezo wote ulikuwa wa kizembe sana na kupoteza mpira mwingi.”

Tuna mengi ya kuchambua. Timu iko tayari kujifunza. Ninaelewa kuwa baadhi ya mambo bado hayajafanyika. Yote kwa yote, ni mabadiliko mengi ambayo yalifanya maisha kuwa magumu kwetu. Tunataka kumiliki mpira. Alisema Tuchel.

Tuchel Anaona Wigo Mpana wa Kuiboresha Bayern Licha Ushindi Mwepesi wa Klassiker

Kufukuzwa kwa Nagelsmann kulikuja licha ya Bayern kuwa katika robo fainali ya Ligi ya Mabingwa. Kila mtu anafahamu kilichokuwa hatarini hapa ni mabadiliko ya kocha ambayo huleta machafuko kwani kulikuwa na mengi ya kuchukua.

Nia ya kutekeleza kila kitu ilikuwepo kwa asilimia 100. Hilo ndilo la muhimu zaidi. Tulipocheza kwa utulivu na uwazi, tulipata nafasi za hali ya juu. Tuna viongozi, na hiyo itatupa amani na kujiamini. Alimaliza hivyo kocha huyo.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.