Kevin De Bruyne anaamini ushindi wa Manchester City wa 4-1 dhidi ya Liverpool Jumamosi ulionyesha wanaweza kumudu bila uwepo wa Erling Haaland.

Mshambuliaji huyo wa Norway Haaland, ndiye anaongoza chati za ufungaji mabao katika Ligi kuu ya Uingereza akiwa na mabao 28 msimu huu, alikosa pambano na Wekundu hao kutokana na jeraha.
Licha ya kutokuwepo kwake, vijana wa Pep Guardiola bado walifanya fujo kwenye Uwanja wa Etihad ili kuendeleza shinikizo kwa Arsenal katika mbio za ubingwa.
Kwa De Bruyne, ushindi huo uliimarisha pendekezo la City kuweza kustahimili bila mchezaji wao chaguo la kwanza, huku Mbelgiji huyo akielekeza kwa mshindi wa Kombe la Dunia wa Argentina, Julian Alvarez kama mwanafunzi anayefaa sana.

Aliiambia tovuti ya City: “Erling ni mchezaji wa ajabu, lakini tumekuwa tukishinda mechi nyingi katika miaka minane iliyopita ambayo nimekuwa hapa. Ni sehemu ya ziada ambayo inatusaidia sana lakini tunajua kama hayupo tuna Julian, ambaye ni mshindi wa Kombe la Dunia. Sidhani kama ni mbadala mbaya tulionao kama mwenza. Kila mtu anajua kazi yake na yeyote aliye uwanjani ataifanya kazi hiyo.”
Matokeo hayo yameifanya City kusalia kwa pointi nane nyuma ya The Gunners wakiwa na mchezo mkononi huku wakilenga kuwasogeza kileleni.
Ingawa nafasi zao za ubingwa haziko mikononi mwao kiufundi, De Bruyne bado anatarajia mabingwa hao wataisukuma Arsenal kila wakati kwani wanashiriki pia Kombe la FA na Ligi ya Mabingwa.

Aliongeza kuwa ni wazi wanajua wako nyuma, bado wanafanya kazi nzuri na wanacheza katika mashindano matatu. Kuwa katika hatua hiyo ya msimu na kuwa hapo inamaanisha kuwa umekuwa thabiti.
“Katika ligi, Arsenal wamekuwa bora kidogo kuliko sisi lakini tunaweza kujaribu na kushinda mechi nyingi iwezekanavyo na kuona tutaishia wapi.” Alimaliza hivyo KDB.

