Kocha wa zamani wa Milan Stefano Pioli amehusishwa na kutaka kuinoa klabu ya Saudi Pro League ya Al-Nassr, ambayo kwa sasa ina wachezaji kama Cristiano Ronaldo, Sadio Mané, Aymeric Laporte na kiungo wa zamani wa Inter, Marcelo Brozovic.

Kwa mujibu wa ripoti kutoka kwa mwanahabari wa Saudi Falahsport na kituo cha Italia Calciomercato.com, Al-Nassr wako mbioni kumfukuza kazi kocha wao wa sasa Luis Castro, na wamempanga Pioli kama mrithi wake.
Pia meridianbet inatoa michezo ya kasino ya mtandaoni kama vile, Aviator, poker, Roullette, sloti na mingine kibao. Ingia meridianbet na ucheze sasa.
Castro huenda akaondolewa majukumu yake baada ya mchezo ujao dhidi ya Al-Ahli siku ya Jumamosi.

Pioli, ambaye alishinda taji la Serie A na Rossoneri msimu wa 2021-22, amekuwa akipatikana tangu mwisho wa msimu uliopita, wakati yeye na Milan waliamua kuachana.
Kulingana na ripoti za leo, Pioli bado yuko kwenye mkataba kiufundi na Milan, ambao hawakukubali malipo ya kifedha wakati kocha huyo alipoondoka mwishoni mwa msimu uliopita.


