Gazeti la Tuttosport linaripoti kuwa Juventus wako kwenye mazungumzo na beki wa Real Madrid Antonio Rudiger, ambaye anapatikana kwa uhamisho wa bure huku mkataba wake ukitarajiwa kuisha mwezi Juni.

Juventus FC wanamuwania beki wa kati wa Real Madrid CF, Antonio Rudiger, na kwa mujibu wa Tuttosport, vigogo hao wa Serie A tayari wameanza mazungumzo na nyota huyo wa kimataifa wa Ujerumani ambaye mkataba wake na Los Blancos unaisha mwezi Juni.
Kocha wa Bianconeri, Luciano Spalletti, ni shabiki mkubwa wa beki huyo mwenye uzoefu. Wawili hao waliwahi kufanya kazi pamoja katika AS Roma kuanzia mwaka 2015 hadi 2017, ambapo Rüdiger alicheza mechi 54 katika dimba la Olimpico chini ya kocha huyo wa Italia.
Kwa mujibu wa ripoti hiyo, Liverpool na Manchester United pia wameonyesha nia ya kujua upatikanaji wa beki huyo, lakini United wanatarajiwa kujiondoa kwenye mbio hizo iwapo watafikia makubaliano ya kuongeza mkataba wa Harry Maguire.

Juventus wanaripotiwa kuwa tayari kumpa Antonio Rudiger mkataba wa miaka mitatu wenye thamani ya kati ya €5m hadi €6m kwa msimu.
Mustakabali wa beki huyo katika Real Madrid bado haujathibitishwa, ingawa nyota huyo wa zamani wa AS Roma hivi karibuni amerejea kwenye kikosi cha kuanzia chini ya Álvaro Arbeloa.
Iwapo Mreno huyo ataendelea kuiongoza Real Madrid msimu wa 2026-27, atamshauri klabu kuongeza mkataba wa Antonio Rudiger.

