Mshambuliaji wa klabu ya Barcelona, Philippe Coutinho anatarajia kuweka wazi mustakabali wake ndani ya klabu hiyo baada ya kuwa ameshafanya maamuzi yake binafsi.

Klabu ya Aston Villa ni moja ya vilabu ndani ya EPL vinavyowania saini ya mchezaji huyo anayetaka kurejea Uingereza kuweza kupata muda wa kucheza zaidi.
Coutinho anasemekana yupo tayari kujiunga na Aston Villa wanaoshikilia nafasi ya 13 katika msimamo wa ligi ya EPL kwakuwa klabu hiyo ina mipango bora zaidi.
Coutinho pia anafahamiana na meneja wa sasa wa Villa, Steven Gerrard ambaye walicheza pamoja kwa misimu miwili na nusu wakiwa Liverpool na hiyo inaweza kuwa sababu nyingine kujiunga na klabu hiyo.
Philippe alisajiliwa Barcelona akitokea Liverpool kwa rekodi ya klabu ya dau la £146m mwezi January mwaka 2018 lakini alishindwa kufanya vizuri Camp Nou kutokana na majeraha.
Una Kila sababu ya kufurahia wiki yako na kutengeneza mwaka huu uwe wa faida zaidi katika kasino zetu za mtandaoni za meridianbettz. Mchezo wa Zeus Ancient Fortunes unakuongoza kutekeleza hilo.


