Kwa mujibu wa ripoti kutoka Ufaransa, Inter wameafikiana masharti binafsi na winga wa Olympique Marseille, Luis Henrique, kwa mkataba hadi Juni 2030.

Tayari kulikuwa na taarifa kadhaa kwamba walikuwa katika mazungumzo na mchezaji huyo, ambaye alikuwa na nia ya wazi ya kuhamia San Siro badala ya Bayern Munich.
Pia meridianbet inatoa michezo ya kasino ya mtandaoni kama vile, Aviator, poker, Roullette, sloti na mingine kibao. Ingia meridianbet na ucheze sasa.
Sasa Footmercato wanadai kwamba Nerazzurri wamekamilisha masharti binafsi kwa mkataba wa miaka mitano utakaoisha Juni 2030.
Klabu bado inahitaji kukubaliana kuhusu masharti ya malipo na Olympique Marseille ili kumnunua mchezaji huyo, lakini tayari wamewasilisha pendekezo lenye thamani ya €24m pamoja na bonasi ya €4m.
Inter wanatarajia kuwa Luis Henrique atakuwa tayari kuichezea timu hiyo kwenye Kombe la Dunia la Klabu litakaloanza katikati ya Juni hadi Julai, wakitumia dirisha la ziada la usajili.


