Klabu ya Kagera Sugar imefikia makubaliano ya kuvunja mkataba na mchezaji wao Abdul Aziz Makame baada ya kuitumikia klabu hiyo kwa muda sasa.

Makubaliano hayo yamefikiwa hii leo April o4 huku mchezaji huyo akiwa alisaini mkataba wa miaka miwili na klabu yao toka mwaka jana mwezi wa saba na kuitumikia hadi sasa ambapo wameachana.
Abdul Aziz Makame alikuwa akicheza nafasi ya kiungo klabuni hapo lakini alikuwa sio chagu tegemezi kwenye kikosi hicho cha wanankurukumbi ambao makazi yao yapo mkoani Kagera.

Klabu imetoa taarifa hiyo ya kuvunja mkataba katika ukurasa wao wa Instagram wa Kagera Sugar na pia inamshukuru sana Makame kwa huduma yake ambayo ameitoa klabuni hapo kwa kipindi chote cha msimu mmoja alipokuwa akiitumikia klabu hiyo na wanamtakia kila la kheri katika maisha yake ya soka huko aendako.
Wanankurukumbi wapo nafasi ya 7 baada ya michezo 25 ambayo wamecheza, wameshinda michezo yao 8, sare 8, na kupoteza michezo 9, na wamejikusanyia pointi zao 32.

