Klabu ya KMC watacheza michezo ya Play-Off ili kubaki ligi kuu ya NBC msimu ujao licha ya kushinda hii leo dhidi ya Mbeya City ugenini.

KMC ameshinda bao 1-0 katika dakika ya kwanza ya mchezo, bao ambalo limetupiwa kimyani na Kulwa lakini hiyo yote haijatosha timu hiyo kusalia ligi kuu na hivyo wanahitajika kucheza michezo ya ziada.
Mbeya City ambao nao wamepoteza hii leo mbele ya vijana wa Julio Kihwelu watatakiwa kucheza play-Off ili wabakie Ligi kuu ambapo wanahitaji nguvu ya ziada.

Je unadahani hawa wote wanaweza kusalia ligi kuu? Au kuna timu moja itatakiwa kumpisha timu kutoka Ligi daraja la kwanza ambao nao pia wanahitaji kucheza Ligi kuu?

