Mlandege Bingwa Mpya Mapinduzi Cup 2023

Hatimaye Bingwa wa Mapinduzi Cup amepatikana hapo jana na si mwingine bali ni Mlandege FC ambaye amechukua Kombe hilo baada ya kumcharaza Singida Big Stars kwa mabao 2-1.

 

Mlandege Bingwa Mpya Mapinduzi Cup 2023

Mlandege amejidhatiti na kuweza kulibakiza Kombe hilo nyumbani kwao huku kipindi cha kwanza pekee kikitosha kuwapa Ubingwa timu hiyo ya visiwani Zanzibar ambapo kabla ya dakika 45 kumalizika walikuwa wamekwisha tupia mabao mawili.

Baada ya kurejea kwa kipindi cha pili vijana wa Pluijm walifunga bao la kwanza ambalo halikutosha kuwapa matumaini ya kubeab kombe hilo kwa mara ya kwanza, na mpaka kipyenga cha mwamuzi kinamalizika timu hiyo ilikuwa tayari imeumaliza mwendo.

Mlandege Bingwa Mpya Mapinduzi Cup 2023

Mlandege mpaka anaingia fainali ameweza kumfunga Simba ambaye ndiye alikuwa bingwa mtetezi, akaja akamfunga Namungo na sasa amemfunga Singida kwenye fainali na hatimaye kutangazwa kuwa ni mabingwa wapya wa Kombe hili.

Mfungaji bora wa michuano hii ni Francy Kazadi, Mchezaji bora Chipukizi Said Mussa Said, Golikipa bora ni Mperule, Mchezaji Bora Yusuf Kagoma.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.