Tanzania Prisons imeendelea kujiweka vizuri kwenye msimamo wa ligi baada ya kushinda mechi yake ya nne mfululizo kwenye ligi kwa kuitandika Kagera Sugar Kaitaba kwa bao 1-0.

Bao hilo la kuipatia Tanzania Prisons pointi tatu za uhakika lilitupiwa kimyani na Edwin Balua kipindi cha pili cha mchezo dakika za lala salama na kuipeleke Prisons hadi nafasi ya 8 kwenye msimamo akiwa na pointi 34.
Baada ya Kagera ya Mexime kupoteza mchezo huo sasa wanabaki katika nafasi ya 7 kwenye msimamo wakiwa na alama zao 35 wakiwa wamesalia na michezo miwili ambayo yote watakuwa ugenini.

Timu hizi zote wamejinusu na kushuka daraja kutokana na nafasi walizopo na hivyo waliopo nafsi kuanzia 13 kushuka chini ndio bado kibarua kipo kwani wataishia kwenye kushuka daraja na wengine kucheza play off.

