Chelsea Wamtolea Macho Maigan.

Mabingwa wa Uefa conference league Chelsea wameonesha uhitaji wa golikipa wa Ac Milan, Mike Maignan huku kocha Enzo Maresca akionesha nia ya kuwa na golikipa namba moja ndani ya kikosi chake kuelekea msimu ujao.

Chelsea Wamtolea Macho Maigan.

Maignan anamaliza mkataba wake na Milan tarehe 30 mwezi huu na inasemekana mpaka sasa bado hajaamua kuongeza mkataba.

Inaelezwa kwamba Maigan anatamani kucheza Klabu bingwa Ulaya na kujitengenezea nafasi kwa timu ya taifa ya Ufaransa, hivyo Ac Milan wanakosa nafasi ya kuendelea nae baada ya kushinda kufuzu kwa ajili ya michuano hiyo kwani wamemaliza nafasi ya nane kwenye msimamo wa ligi.

Kiwango alichokionesha golikipa Robert Sanchez ndani ya Chelsea kimeibua mshtuko miongoni mwa maboss wa timu hiyo hali inayowafanya kuhakikisha waanapata mbadala wake mapema kuelekea michuano ya Ligi ya mabingwa watakayoshiriki msimu ujao mara baada ya kufanikiwa kumaliza ndani ya nafasi tano za msimamo wa ligi kuu nchini Uingereza.

Chelsea Wamtolea Macho Maigan.
 

Hii si mara ya kwanza kwa Chelsea kumtaka Maigan kwani hata kwa misimu kadhaa nyuma wamekua wakionesha malengo ya kumuhitaji ingawa hawakufanikiwa na sasa wameliwekea nguvu suala hilo na wanaoangaliwa hivi sasa ni Milan kumruhusu golikipa huyo aondoke.

Maigan mwenye umri wa miaka 29 msimu huu amecheza jumla ya michezo 37 ya ligi akiruhusu kufungwa mabao 38, wastani wa goli moja kwa kila mchezo na amecheza jumla ya michezo 12 bila kuruhusu bao lolote lile huku akiokoa matukio ya hatari 100.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.