Christian Atsu amepatikana akiwa amefariki baada ya tetemeko la ardhi lililoikumba Uturuki na taarifa hiyo imetoka ndani ya klabu yake inayoshiriki Super Lig Uturuki.

Mchezaji huyo wa zamani wa Ligi kuu ya Uingereza alikuwa hajaonekana tangu kusini mwa Uturuki na kaskazini mwa Syria kukumbwa na tetemeko kubwa Februari 6.
Hapo awali akiwa na Newcastle United, Chelsea na Everton, Atsu aliifungia Hatayspor siku moja kabla ya tetemeko hilo, ambalo lilisababisha kuporomoka kwa jengo la ghorofa alimokuwa akiishi mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 31.
Hapo awali klabu ya Christian iliripoti kwamba alikuwa ametolewa kwenye vifusi, lakini ikathibitishwa kwamba haikuwa hivyo. Taarifa za Hatayspor zilisema mwili wa Atsu sasa umepatikana na unarejeshwa katika nchi yake ya Ghana.

Klabu hiyo ilisema katika taarifa iliyotumwa kwenye mtandao wa kijamii: “Mazishi ya mchezaji wetu wa kandanda Christian Atsu, ambaye alipoteza maisha chini ya kifusi, yako njiani kutumwa katika mji aliozaliwa huko Ghana.”
Klabu hiyo imeandika hivi; “Hatutakusahau Atsu, Amani iwe juu yako mrembo. Hakuna maneno ya kuelezea huzuni yetu. REST in PEACE ATSU.”

Zaidi ya watu 40,000 wameripotiwa kufariki kutokana na matetemeko ya ardhi na mamlaka za mitaa.

