David Moyes amefichua kuwa tayari alikuwa ameweka wazi msimamo wake kwa nahodha wa zamani wa Aston Villa, Jack Grealish, kufuatia mchezaji huyo wa kiungo kushushwa kwa kadi nyekundu katika mechi dhidi ya Wolves.

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 30 alionyeshwa kadi mbili za njano, zote kwa kosa la kulalamika (dissent), katika dakika za mwisho za mchezo huku Everton wakijitahidi kwa nguvu zote kulinda pointi moja dhidi ya timu iliyoko mkiani mwa msimamo wa Ligi Kuu England.
Kadi hizo zilikuja muda mfupi baada ya Michael Keane naye pia kutolewa nje kwa kadi nyekundu, baada ya mwamuzi Thomas Kirk kuamua kuwa alihusika katika kitendo cha utovu wa nidhamu (violent conduct), alipodaiwa kumvuta nywele mshambuliaji Tolu Arokodare.
Matokeo ya kadi hizo yaliwaacha Everton wakiwa na wachezaji tisa pekee uwanjani, huku wakipambana kuepuka kipigo kwa dakika tisa za nyongeza, jambo lililoongeza matatizo kwa klabu hiyo baada ya mambo kuanza kwenda vibaya pale Mateus Mané alipofunga bao la kusawazisha dakika ya 69.



