Mwenyekiti wa West Ham David Sullivan amethibitisha kuwa nahodha Declan Rice ataruhusiwa kuondoka msimu huu wa joto na anatarajia kuanza kupokea ofa mara moja.

Kiungo huyo wa kati wa Uingereza alisema hajui kama aliichezea klabu hiyo mechi yake ya mwisho baada ya kuiongoza kutwaa ubingwa wa Ligi ya Europa.
Ushindi wa 2-1 dhidi ya Fiorentina katika fainali ya hapo jana usiku ulimfanya kuwa nahodha wa tatu wa Hammers kunyanyua kombe kuu, akiwafuata Bobby Moore na Billy Bonds.
Hata hivyo, Sullivan anakubali makubaliano ya kiungwana yanamaanisha kuwa watamruhusu mchezaji ambaye bado ana miaka miwili kwenye mkataba wake mwaka mmoja pamoja na chaguo la kuondoka.

Alipoulizwa kama kunyanyua kombe huko Prague ilikuwa hatua ya mwisho ya Rice kama mchezaji wa West Ham, Sullivan aliiambia talkSPORT: “Nadhani lazima iwe hivyo. Tulimuahidi kwamba anaweza kwenda. Aliweka moyo wake kwenda na kwa wakati unaofaa lazima aende na lazima tupate mbadala.”
Sio jambo ambalo tulitaka litokee. Tulimpa pauni 200,000 kwa wiki miezi 18 iliyopita na alikataa. Huwezi kuweka mchezaji ambaye hataki kuwepo. Nadhani ofa zitaanza kuja leo. Vilabu vitatu au vinne vimeonyesha nia lakini, kwa heshima na West Ham, wakati sisi bado tunacheza, hautoi ofa kwa wachezaji. Alisema Sullivan
Rice alisema baada ya mchezo kuwa bado si kwaheri na aliongeza kuwa kuna uvumi mwingi kuhusu mustakabali wake. Kuna vilabu vingi vinamtaka lakini bado yeye ana miaka mwili aliyobakiza West Ham.

“Ninapenda kila dakika ya hapa, unaweza kuona tabasamu usoni mwangu. Sio kuhusu hilo usiku wa leo, ni kuhusu kusherehekea na ndivyo nitafanya sasa.”

