Michele Criscitiello anapendekeza kwamba Everton wanakaribia kufikia makubaliano ya kumnunua winga wa Leeds United Wilfried Gnonto.

 

Everton Wanakaribia Kumnunua Winga wa Leeds United Gnonto

Mtaliano huyo mwenye umri wa miaka 19 alijiunga na timu ya Uingereza kutoka FC Zurich Septemba iliyopita kwa mkataba wa thamani ya karibu €4.5m, akitia saini kandarasi ya miaka mitano.


Meridianbet inaendelea kutoa promosheni na mchezo wake wa kasino ya mtandaoni Aviator ambao utakufanya wewe usafiri kuelekea kivutio cha utalii chochote ukipendacho baada ya kuwa mshindi. Hivyo hii nayo isikupite cheza sana.

Nafasi zilikuwa finyu kwa Gnonto huku kukiwa na msukosuko wa msimu huko Leeds, lakini alipokuwa uwanjani alivutia, akifunga mabao manne na kutoa pasi nne za mabao katika jumla ya mechi 28.

Everton Wanakaribia Kumnunua Winga wa Leeds United Gnonto

Kama ilivyoripotiwa na Criscitiello wa SportItalia, Everton sasa wanakaribia kufikia makubaliano na Gnonto, tayari kuilipa Leeds takriban euro milioni 22.

Leeds walimaliza katika nafasi ya 19 kwenye msimamo wa Ligi Kuu msimu uliopita, hivyo kuwashusha kwenye michuano hiyo, hivyo wachezaji kadhaa wameuzwa ili kusaidia kupunguza gharama katika klabu hiyo.

Gnonto tayari ameshaichezea timu ya taifa ya Italia mechi 12 na anaonekana atakua mchezaji bora katika miaka ijayo, na kufanya usajili huo kuwa mzuri na Everton.


JIBU

Tafadhali andika maoni yako
Tafadhali andika jina lako hapa