Vyanzo vingi vinaripoti kuwa Fiorentina wamekubali dili la thamani ya €10m pamoja na bonasi kwa beki wa kushoto wa Empoli, Fabiano Parisi.

Sportitalia, Sky Sport Italia na RAI Sport zote zina imani kuwa klabu hizo mbili zimefanyia kazi maelezo yote.
Itakuwa €10m na takriban €1m kwa nyongeza, wakati mchezaji tayari amekubaliana na Viola kwa mkataba wa miaka mitano.
ODDS KUBWA, machaguo zaidi ya 1000, mechi mubashara na mechi zote Duniani zinapatikana Meridianbet pekee, unasubiri nini sasa?. Ingia na ucheze michezo yote uipendayo na ushindi ni wazi wazi.

Parisi sasa anatakiwa kufanyiwa uchunguzi wa kimatibabu katika siku chache zijazo, kwani vijana wa Vincenzo Italiano wanatarajiwa kuanza mazoezi ya kabla ya msimu mpya.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 22 pia alikuwa akilengwa na Juventus na Torino, lakini Tuscans walikuwa wazuri zaidi na wakali katika mbinu yao.
Rais wa Empoli Fabrizio Corsi pia alithibitisha leo kuwa walikuwa wakingojea ofa sahihi kutoka Fiorentina na ilifika jioni ya jana.

Akiwa mchezaji wa akademia ya Benevento na Avellino, alihamia Empoli kwa €450,000 mnamo Septemba 2020.
Msimu uliopita, Parisi alichangia mabao mawili na asisti mbili katika mechi 33 za Serie A na aliichezea Italia katika Mashindano ya Ubingwa wa U-21.

