Shirikisho la soka duniani FIFA limetangaza kuwa Japan imejiondoa katika haki ya kuandaa mashindano ya klabu bingwa dunia kwa sababu ya kuongezeka kwa kesi za Covid-19 nchini humo.

Taarifa ilisomeka: “FIFA inaweza kuthibitisha kwamba imearifiwa leo na Chama cha Soka cha Japani (JFA) kwamba, kwa sababu ya janga la COVID-19 na hali ya mwenyeji nchini, hawana nafasi tena ya kukaribisha Klabu Bingwa Dunia 2021.
“FIFA inapenda kuwashukuru JFA kwa kazi yao na kujitolea kwao na wanatarajia kurudi Japan baadaye. Maelezo zaidi kuhusu mwenyeji mbadala wa Kombe la Klabu Bingwa Dunia la 2021 yatatangazwa kwa wakati ufaao.”
Inabakia kuonekana mahali ambapo mashindano hayo yatakafanyika lakini kulingana na ESPN, inaweza kuhamishiwa Qatar kama mtangulizi wa kuandaa Kombe la Dunia la 2022.
Meridianbet inakuletea ushindi kwenye kiganjani kwako, unafurahia radha halisi ya burudani ya kasino mtandaoni na tabasamu la ushindi.


