Kocha mkuu wa Lazio Maurizio Sarri amemkosoa vikali mwamuzi Craig Pawson aliyemtoa kwa kadi nyekundu Patric katika kipindi cha kwanza dhidi ya Cluj, akisema mwamuzi huyo wa Uingereza hastahili kuchezesha mechi za Ulaya.

Biancocelesti walipata ushindi wa 1-0 katika mkondo wa kwanza wa mchujo wa Ligi ya Konferensi kwenye Uwanja wa Stadio Olimpico hapo jana kutokana na bao la Ciro Immobile. Hata hivyo, walilazimika kucheza takribani mechi nzima wakiwa na wachezaji 10 kwa sababu ya kadi nyekundu ya moja kwa moja aliyoonyeshwa beki wao Patric baada ya dakika 15 pekee.
Faulo ya Patric ilikuwa yadi 10-15 nje ya eneo la hatari huku mabeki wengine wa Lazio wakiwa karibu na mpira, lakini Pawson bado aliiona kuwa nafasi ya wazi ya kufunga. Ni salama kusema Sarri hakukubaliana na mwamuzi wa Kiingereza.

Sarri amesema kuwa; “Kitu pekee ninachoweza kusema ni kwamba ni jambo lisilofikirika kuwa anaongoza katika ngazi ya Ulaya. Immobile alifunga bao gumu, lakini ni nyumba maalum. Natumai itachangia kumtoa ukungu kichwani. Katika usiku ambao kila kitu kilionekana kuwa kinakwenda kinyume, tulipata matokeo yanayokubalika.”
Sarri aliendelea kumlaumu Pawson wakati wa mkutano wake na waandishi wa habari baada ya mechi akisema kuwa huyo ni mwamuzi ambaye hawezi kuzunguka Ulaya kuchezesha michezo, hafai kabisa. Alibadilisha mchezo kwa kadi nyekundu ambayo haikuwa nafasi ya wazi ya kufunga na kuendelea na kadi za njano za kushangaza. Natumai ni mwamuzi maskini tu.

Biancocelesti watacheza mkondo wa pili ugenini wiki ijayo. Wanacheza Ligi hiyo baada ya kutolewa kwenye Ligi ya Europa, na kumaliza nafasi ya tatu kwenye kundi lao.

