Erik ten Hag aliachwa akiuguza majeraha wakati Manchester United ikipata huzuni ya dakika za lala salama dhidi ya Sevilla kwenye Ligi ya Europa, huku Marcel Sabitzer akipiga mabao mawili ya uongozi.

Mabao mawili ya Sabitzer katika kipindi cha kwanza yalionekana kuwafanya United kuwa na udhibiti kamili wa mkondo wa kwanza wa robo fainali ya jana, huku wenyeji Ten Hag wakiwa na nguvu kubwa katika uwanja wa Old Trafford.
Bao la kujifunga la Tyrell Malacia dakika sita kabla ya mchezo kumalizika liliwapa matumaini Sevilla kabla ya Harry Maguire kuachia wavu wake dakika ya 92. Ten Hag alisisitiza kuwa sare ya 2-2 ya United ilikuwa chini kwa bahati mbaya, tofauti na wachezaji wake wa akiba kuzimia kwa shinikizo la dakika za mwisho.
Kocha wa United aliiambia BT Sport: “Nadhani tulikuwa na mchezo mkononi, tulikuwa mbele kwa mabao 2-0 na tungefunga mabao matatu au manne. Mchezo ulikuwa juu yetu kabisa.”

Ten Hag amesema kuwa anajua wanaweza kufanya vizuir zaidi wakiwa na wachezaji hao katika sehemu ya mwisho ya mchezo ilibidi wawe watulivu zaidi na waweze kufaidika na nafasi zao za kushambulia lakini hawakufanya hivyyo.
“Hatukuwa na bahati kidogo na safu ya ulinzi, mabao mawili ya kujifunga wenyewe na mikwaju ya kupangua, sio usiku mzuri.”
Mchezo wa jana uliifanya United kuwa timu ya pili ya Uingereza kujifunga mabao mawili pekee katika mechi moja kwenye mashindano makubwa ya Ulaya, baada ya Chelsea dhidi ya Ajax ya Ten Hag mnamo Novemba 2019.

Ilikuwa pia mara ya kwanza kwa United kushindwa kushinda mechi katika michuano mikubwa ya Ulaya walipoongoza kwa mabao mawili kwa moja, tangu sare ya 3-3 na Basel Septemba 2011.
Sabitzer aliiambia BT Sport; Tulicheza kipindi kizuri cha kwanza, tulipata nafasi nzuri baada ya hapo na tulilazimika kumaliza mchezo kwa mbali. Mwisho ni sare na sivyo tulivyotaka hivyo lazima twende Sevilla na kufanya hivyo. Kwa bahati mbaya tulitoa mabao mepesi, hatuwezi kuruhusu mabao ya aina hii na tumesikitishwa sana sasa.”
Mchezaji huyo aliongeza kwa kusem akuwa katika shindano la namna hiyo lazima uwe makini hadi mwisho, unapokuwa na asilimia ndogo unaweza kutoa mchezo, na anadhani dakika za mwisho zilikuwa za kushangaza, mtu mmoja alishuka na ilibidi wapate matokeo.

United watatarajia kupambana katika mechi ya marudiano kwenye Uwanja wa Ramon Sanchez-Pizjuan, ingawa Mashetani Wekundu wanakabiliwa na wasiwasi kuhusu utimamu wa beki wao wa kati Varane na Martinez.
Ten Hag alipendekeza Varane aliongeza jeraha ambalo lilimweka nje ya uwanja baada ya mapumziko ya kimataifa ya Machi, wakati Mholanzi huyo alikuwa na wasiwasi kwamba Martinez alishuka uwanjani licha ya kutokuwa na mpinzani yoyote.

