Lionel Messi amerejea mazoezini na klabu ya Paris St Germain kufuatia kusimamishwa kwake kwa safari isiyoidhinishwa ya kwenda Saudi Arabia.

Klabu hiyo ya Ligue 1 ilithibitisha kwenye akaunti yao rasmi ya Twitter leo hii asubuhi kwamba mchezaji huyo wa kimataifa wa Argentina mwenye umri wa miaka 35 alirejea kwenye kundi baada ya kupigwa faini na kusimamishwa kwa kufanya ziara ya kujitangaza katika nchi hiyo ya Mashariki ya Kati bila ruhusa.
Chapisho hilo, ambalo liliambatana na picha ya mshindi wa Kombe la Dunia katika jezi za mazoezi, lilisema kwa urahisi: “Leo Messi amerejea mazoezini Jumatatu asubuhi.”
Messi, ambaye ni balozi wa Mamlaka ya Utalii ya Saudia, alipigwa picha mjini Riyadh siku moja baada ya timu yake kushindwa na Lorient.

Baadaye alifichua katika video iliyowekwa kwenye akaunti yake rasmi ya Instagram kwamba alilazimika kufanya safari hiyo kwa sababu za kimkataba, baada ya kughairi hapo awali, na alidhani kuwa alikuwa na siku ya kupumzika.
Messi alisema: “Nilitaka kutengeneza video hii kutokana na kila kitu kinachoendelea. Kwanza kabisa, nataka kuwapa pole wachezaji wenzangu na klabu. Kwa kweli nilifikiri kwamba tungekuwa huru baada ya mchezo, kama ilivyokuwa katika wiki zilizopita.”
Nilikuwa nimepanga safari hii kwenda Saudi Arabia, ambayo ilikuwa imeghairiwa hapo awali na wakati huu sikuweza. Naomba radhi tena na niko hapa kwa lolote ambalo klabu itaamua. Kila la kheri. Alisema Messi.

Mshindi huyo mara saba wa Ballon d’Or alijiunga na PSG kutoka Barcelona mnamo Agosti 2021 baada ya klabu hiyo ya Catalan kukumbwa na matatizo makubwa ya kifedha na, ingawa kurejea kumetajwa, matatizo hayo yanafanya hilo lisiwezekane.
Katika siku za hivi majuzi, amekuwa akihusishwa na kuhamia kwenye Ligi ya Pro ya Saudi Arabia huku kukiwa na ripoti kwamba anaweza kupata hadi pauni milioni 320 kwa mwaka.

