Klabu ya PSG imetangaza kuwa Neymar amefanikiwa kufanyiwa upasuaji kwenye jeraha lake la kifundo cha mguu ambalo litamuweka nje msimu huu mzima.

Mbrazil huyo amekuwa nje ya uwanja tangu kutolewa katika ushindi wa 4-3 wa Ligue 1 dhidi ya Lille mwezi uliopita.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 31 amekuwa akifurahia msimu wake wenye tija zaidi kwa PSG tangu kampeni ya 2018-19, sawa na hesabu ya mabao 34 ya moja kwa moja (mabao 18, asisti 16) katika mashindano yote akiwa wa pili kwa juu zaidi katika maisha yake ya PSG na nyuma ya 44 katika msimu wake wa kwanza.

PSG wameshinda mechi zao zote mbili za Ligue 1 bila Neymar na hivyo kusonga mbele kwa pointi nane kileleni kwenye msimamo, ingawa waliondolewa kwenye Ligi ya Mabingwa kufuatia kichapo cha 2-0 kutoka kwa Bayern Munich Jumatano.
Kocha mkuu Christophe Galtier alithibitisha mapema wiki hii kwamba Neymar atakosa msimu uliosalia, huku mshambuliaji huyo akitarajiwa kuwa nje kwa miezi mitatu hadi minne.

Taarifa ya klabu iliyotolewa jana ilisomeka: “Neymar amefanyiwa upasuaji Ijumaa alfajiri katika Hospitali ya ASPETAR mjini Doha, na Maprofesa Pieter D’Hooghe, James Calder na Rodrigo Lasmar.”

