Nyota wa Roma, Tammy Abraham anakiri Ureno inamtaka José Mourinho lakini anasisitiza kuwa kipekee analenga tu Roma na yeye ndiye kocha anayemhitaji.

Shirikisho la Ureno linasemekana kuwa lilianzisha mazungumzo na wakala wa Mourinho, Jorge Mendes, kuhusu uteuzi wa kuwa kocha wa timu ya Taifa. Ureno ilitinga robo fainali kwenye Kombe la Dunia, na kumtimua Fernando Santos na Mourinho sasa ndiye mgombea anayeongoza kuchukua nafasi yake.
Abraham hashangazwi na maslahi ya Shirikisho la Ureno, na amesema kuwa;
“Yeye ni kocha mzuri na bila shaka, kila mtu anamtaka, heshima kwamba nchi muhimu kama Ureno inamfukuza. Nina hakika kwamba kocha analenga Roma. Tumesoma mambo mengi, lakini hatukuzungumza kuyahusu na Mourinho amejaribu kila mara kutuboresha, tunazingatia msimu.”

Abraham anasema kuwa tayari alisema hapo awali kwake Mourinho hapo ni kama mjomba na hivyo ndivyo amekuwa akimuona kocha huyo. Yeye ni sehemu ya kumbukumbu na wanataka bora kutoka kwake kwahiyo anamtia moyo kila njia.
“Ananiambia nisipocheza vizuri na hata ninapofanya hivyo, haridhiki. Hiyo ndiyo ninayohitaji. Kocha ambaye ananiongoza kila wakati.”
Roma iliifunga RKC katika mechi ya kirafiki siku ya Alhamisi, mchezo ambao ulimfanya Abraham kupata jina lake kwenye ukurasa wa mabao.
Anasema kuwa, yote yalikuwa mazuri nchini Ureno. Ni furaha kufunga Roma, klabu muhimu sana maishani mwake na wana matumaini kuelekea sehemu ya pili ya msimu, wanatazamia kuanza tena.

Giallorossi wataanza tena msimu Januari 4, wakiwa nyumbani dhidi ya Bologna. Wako pointi 14 chini ya vinara wa msimamo ambao ni Napoli na pointi tatu kutoka kwenye nafasi nne za juu. Je, Roma wataweza kupata nafasi ya kucheza Ligi ya Mabingwa msimu huu?
“Tutafanya kila tuwezalo na tutaona kitakachotokea, lakini nadhani hivyo,” mshambuliaji huyo alihitimisha.

