Vipimo vilivyofanyiwa Giovanni Di Lorenzo vimeondoa hofu ya jeraha kubwa la goti, na kwa kuwa muda wa kupona unatarajiwa kuwa kati ya siku 40 hadi 60, Italia na Gennaro Gattuso wanatumaini beki huyo mwenye uwezo wa kucheza nafasi nyingi atakuwa tayari kwa mechi ya mchujo ya Kombe la Dunia mwezi ujao.

Beki wa Napoli, Di Lorenzo, huenda akapatikana kwa mechi ya mchujo ya Kombe la Dunia ya Italia mwezi ujao. Beki huyo wa Azzurri alitolewa nje wakati wa mechi ya mwisho ya Serie A ya Napoli dhidi ya Fiorentina.
Awali, Partenopei waliogopa kuwa Di Lorenzo alikuwa amepata jeraha la mishipa ya goti, lakini vipimo vilivyofanyika Villa Stuart siku ya Jumatatu vilibainisha kuwa ana sprain ya daraja la pili kwenye goti la kushoto.
Hii ina maana kwamba Di Lorenzo ataendelea kuwa nje ya uwanja kwa takribani siku 40 hadi 60, kwa kuwa hatofanyiwa upasuaji bali atafuata matibabu ya kawaida (yasiyo ya upasuaji).
Meridianbet inakwambia kuwa endelea kubashiri hapa kwani ODDS KUBWA na machaguo zaidi ya 1000 yapo hapa. Ingia kwenye akaunti yako na uanze safari yako ya ushindi sasa.


