Mvutano mkubwa umeibuka kati ya Ukraine na Rais wa FIFA, Gianni Infantino, baada ya kiongozi huyo wa soka duniani kupendekeza uwezekano wa kuondoa marufuku kwa Urusi katika mashindano ya kimataifa. Waziri wa Michezo wa Ukraine, Matvii Bidnyi, amemshambulia Infantino vikali, akimuita asiye na uwajibikaji na mwenye kauli za kitoto, akisisitiza kuwa soka haliwezi kutenganishwa na uhalisia wa vita vinavyoendelea.
Urusi ilisimamishwa kushiriki mashindano yote ya FIFA na UEFA tangu Februari 2022 kufuatia uvamizi wake nchini Ukraine. Hata hivyo, Infantino amesema marufuku hiyo haijafanikisha chochote bali imezalisha hasira na chuki zaidi, akidai kuwa kuruhusu watoto wa Urusi kucheza soka Ulaya kungeleta mwelekeo chanya. Kauli hizo ndizo zilizomchochea Bidnyi kujibu kwa ukali kupitia mitandao ya kijamii.
“Maneno ya Gianni Infantino yanasikika kuwa hayana uwajibikaji, kama si ya kitoto kabisa,” alisema Bidnyi. “Yanalitenganisha soka na uhalisia ambao watoto wanauawa. Tangu mwanzo wa uvamizi kamili wa Urusi, zaidi ya wanamichezo na makocha 650 wa Ukraine wameuawa, wakiwemo zaidi ya wachezaji 100 wa soka.” Kauli hiyo imeongeza uzito wa mjadala juu ya nafasi ya michezo wakati wa vita.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa




