Kiungo wa kati wa Udinese Sandi Lovric aionya Napoli kwamba Bianconeri ‘wanataka kushinda’ siku ya Alhamisi wakati Partenopei wanaweza kuweka mikono yao kwenye taji la Serie A lililokuwa likisubiriwa kwa muda mrefu.

Partenopei ilitoka sare ya 1-1 na Salernitana siku ya Jumapili na kulazimika kuahirisha sherehe zao za ubingwa.
Watapata nafasi nyingine hivi karibuni kwani sare ugenini dhidi ya Udinese Alhamisi itatosha kushinda Scudetto. Wanaweza kusherehekea mapema zaidi ikiwa mpinzani wao wa karibu Lazio hatashinda Sassuolo kwenye Uwanja wa Stadio Olimpico Jumatano.
Lovric amesema; “Tunajua hali ilivyo, lakini tuna jambo moja tu akilini, tunataka kushinda. Haijalishi kama Lazio itashinda au kushindwa, tunataka kujitolea kwa kila kitu ili kushinda mbele ya mashabiki wetu. Tunazungumza na tunajua michezo hii ni muhimu kufikia lengo letu, tunajua tunaweza kufaulu.”

Udinese wanashika nafasi ya 13 kwenye Serie A, pointi 13 chini ya Atalanta iliyo nafasi ya 7 na 15 juu ya eneo la kushushwa daraja.

