Luka Modric anaweza kukosa mechi ya fainali ya Copa del Rey ya Real Madrid dhidi ya Osasuna na mkondo wa kwanza wa nusu fainali ya Ligi ya Mabingwa dhidi ya Manchester City baada ya kupata jeraha la paja.

Modric alipata jeraha kwenye mguu wake wa kushoto wakati Madrid ilipochapwa 4-2 na Girona Jumanne, matokeo ambayo yaliwafanya wabaki pointi 11 nyuma ya vinara wa LaLiga Barcelona.
Kipigo hicho kinakuja wakati wa bahati mbaya kwa Los Blancos, ambao watapania kumaliza kungoja kwa miaka tisa ili kubeba Kombe la Mfalme mnamo Mei 6, kabla ya kuwakaribisha City siku tatu baadaye.
Alipoulizwa kuhusu utimamu wa Modric kabla ya mechi ya kesho dhidi ya Almeria, Ancelotti alikiri kupoteza uzoefu wa Mcroatia huyo kungekuwa kikwazo kikubwa.

Ancelotti amesema; Alipata jeraha kwenye mchezo dhidi ya Girona. Tutaona jinsi atakavyoendelea siku chache zijazo. Atakuwa na shaka kwenye fainali ya Copa, lazima tumpime, tumeumia, lakini inaweza kutokea, natumai atapona kwa mechi muhimu. Tuna viungo muhimu sana kama Federico Valverde, Eduardo Camavinga na Aurelien Tchouameni.”
Madrid wameshinda mechi nne pekee kati ya tisa zilizopita za ligi (D2 L3) na kuwaruhusu Barca kujikita kileleni.
Akidai kwa nini Madrid wameshindwa kuiga ushujaa wao wa kombe kwenye LaLiga msimu huu, Ancelotti alisema kuwa hajui ni suala la umakini, ni kawaida, sio kila wakati utaweza kuwa kileleni.

Katika baadhi ya michezo unazingatia vyema zaidi, na katika mingine ni mbaya zaidi. Inatokea kwa kila mtu, siku nzuri na mbaya. Lazima uwaamini wachezaji. Naona kundi likiwa katika hali nzuri. Kilichotokea msimu uliopita hakiwezi kusahaulika na tunataka kurudia. Alimaliza hivyo Carlo

