Xavi Akiri Kuwa Alitaka Kumsajili Nyota wa Arsenal.

Aliyekuwa kocha mkuu wa FC Barcelona, Xavi Hernández, amekiri kuwa aliwahi kumtaja mmoja wa viungo wa sasa wa Arsenal FC kama lengo kuu la usajili wakati alipokuwa akiinoa timu hiyo katika uwanja wa Spotify Camp Nou.

Xavi Akiri Kuwa Alitaka Kumsajili Nyota wa Arsenal.

Mchezaji anayezungumziwa ni Martín Zubimendi. Barcelona walihusishwa kwa muda mrefu na nia ya kumsajili kiungo huyo wa kimataifa wa Hispania wakati alipokuwa akiichezea Real Sociedad. Nia hiyo iliongezeka zaidi baada ya kuthibitishwa kuwa kiungo mkongwe Sergio Busquets angeondoka kuelekea ligi ya Major League Soccer.

Kama ilivyodokezwa hapo juu, mtu aliyekuwa akiongoza wazo hilo la kumleta Zubimendi Barcelona hakuwa mwingine bali Xavi mwenyewe.

Meridianbet inakwambia kuwa endelea kubashiri hapa kwani ODDS KUBWA na machaguo zaidi ya 1000 yapo hapa. Ingia kwenye akaunti yako na uanze safari yako ya ushindi sasa.

Akizungumza katika mahojiano na La Vanguardia katika saa 24 zilizopita, gwiji huyo wa Barcelona aliulizwa kuhusu Zubimendi ambaye sasa anachezea Arsenal.

Xavi Akiri Kuwa Alitaka Kumsajili Nyota wa Arsenal.

Kocha huyo alisema: “Niliuomba uongozi wa Barcelona wamsajili Martín Zubimendi, lakini waliniambia hapana. Ilikuwa ni uamuzi wa kifedha, wakachagua kumsajili mchezaji wa bei nafuu zaidi. Lakini tulikuwa tumempoteza Busquets… nikajiuliza inawezekanaje tusimsajili Zubimendi?”

Kwa kauli hiyo, Xavi ameweka wazi kuwa aliona Zubimendi kama mbadala muhimu wa Busquets wakati alipokuwa akiiongoza Barcelona.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.