Aliyekuwa kocha mkuu wa FC Barcelona, Xavi Hernández, amekiri kuwa aliwahi kumtaja mmoja wa viungo wa sasa wa Arsenal FC kama lengo kuu la usajili wakati alipokuwa akiinoa timu hiyo katika uwanja wa Spotify Camp Nou.

Mchezaji anayezungumziwa ni Martín Zubimendi. Barcelona walihusishwa kwa muda mrefu na nia ya kumsajili kiungo huyo wa kimataifa wa Hispania wakati alipokuwa akiichezea Real Sociedad. Nia hiyo iliongezeka zaidi baada ya kuthibitishwa kuwa kiungo mkongwe Sergio Busquets angeondoka kuelekea ligi ya Major League Soccer.
Kama ilivyodokezwa hapo juu, mtu aliyekuwa akiongoza wazo hilo la kumleta Zubimendi Barcelona hakuwa mwingine bali Xavi mwenyewe.
Meridianbet inakwambia kuwa endelea kubashiri hapa kwani ODDS KUBWA na machaguo zaidi ya 1000 yapo hapa. Ingia kwenye akaunti yako na uanze safari yako ya ushindi sasa.
Akizungumza katika mahojiano na La Vanguardia katika saa 24 zilizopita, gwiji huyo wa Barcelona aliulizwa kuhusu Zubimendi ambaye sasa anachezea Arsenal.


