Inter wanafuatilia kwa karibu wapinzani wao Juventus huku wakipanga mpango wa kumnunua winga nyota Federico Chiesa mwaka ujao.

Mshambuliaji huyo wa Kiitaliano mwenye umri wa miaka 26 ameingia mwaka wa mwisho wa mkataba wake na Bianconeri na bado hajakubali kusaini mkataba mpya, huku kukiwa na kutoelewana juu ya mshahara na urefu wa makubaliano.
Pia meridianbet inatoa michezo ya kasino ya mtandaoni kama vile, Aviator, poker, Roullette, sloti na mingine kibao. Ingia meridianbet na ucheze sasa.

Chiesa amekuwa akihusishwa na kutaka kuondoka Juventus msimu huu wa joto, huku vilabu mbalimbali kama Roma, Chelsea na Tottenham zikiwa na nia ya kutaka kumnunua. Klabu hiyo iliamua kumuacha mchezaji huyo nje ya kikosi chao kwa ajili ya mapumziko ya mazoezi ya kujiandaa na msimu mpya nchini Ujerumani.
Corriere della Sera anapendekeza kwamba Inter wanaangalia kwa karibu hali ya Chiesa huko Juventus huku wakipanga uwezekano wa uhamisho wa bure kwa winga huyo nyota msimu ujao.


