Ni Kama kazinduka kutoka kuzimu nyota Simba Kibu Denis ambaye jana alifunga kwa mara ya kwanza ndani ya ligi kuu baada ya kumaliza siku takribani 380 bila kuona bao.
Lakini Jana dhidi ya Dodoma Jiji aliweka chuma 2 na kutoa assist kwenye ushindi wa 6-0 dhidi ya Dodoma Jiji. Ni mbinu za Kocha Mkuu Fadlu Davids anayekinoa kikosi cha Simba zimejibu wakipata ushindi wa mabao 6-0 dhidi ya Dodoma Jiji mchezo wa Ligi Kuu Bara ikiwa ni mzunguko wa pili kwenye ligi namba nne kwa ubora Uwanja wa KMC, Complex.
Katika mchezo huo ni Ellie Mpanzu alifungua akaunti ya mabao dakika ya 15, Jean Ahoua akatupia mabao mawili dakika ya 21 na 45 huku Steven Mukwala akifunga bao moja dakika ya 47 akiwa ndani ya 18.
Kibu Denis alifunga dakika ya 54 kwa pigo la kichwa akiwa ndani ya 18 na bao la pili katupia dakika ya 69.
Ikumbukwe kwamba Kibu D mara ya mwisho kufunga kwenye ligi ilikuwa katika mchezo dhidi ya Yanga uliochezwa Uwanja wa Mkapa, Novemba 5 2023. Yanga wakishinda 5-1.
Dodoma Jiji inabaki na pointi 27 kwenye msimamo huku Simba ikiwa imefikisha pointi 57 baada ya kucheza jumla ya mechi 22 msimu wa 2024/25.
Kibu akachaguliwa kuwa mchezaji bora wa mchezo baada ya dakika 90 kugota mwisho akiwa kahusika kwenye mabao manne kati ya sita yaliyofungwa na Simba huku Ahoua akifikisha mabao 12 ndani ya ligi ni kinara wa utupiaji.
Vinara wa ligi ni Yanga wenye pointi 58 kibindoni na safu ya ushambuliaji imetupia mabao 58 ndani ya msimu huku washambuliaji wake wawili Prince Dube na Clement Mzize wakiwa na mabao 10 kila mmoja.