KWA YANGA MECHI IPO PALE PALE

Mabosi wa Yanga wamebainisha kuwa hakuna kipengele kwenye mchezo wa Kariakoo Dabi ambao unatarajiwa kuchezwa leo Machi 8 2025, saa 1:15 Uwanja wa Mkapa.

KWA YANGA MECHI IPO PALE PALE

Na Kwamba watakwenda uwanjani Kama kawaida na hakuna siku nyingine yoyote ambayo mechi hiyo itachezwa kama siyo leo kWa kuwa utaratibu wote wa mechi hiyo wao wameshafanya.

Uongozi wa Simba usiku wa kuamkia Machi 8 2025 walitoa taarifa kwamba hawatashiriki mchezo kutokana na kutopewa ruhusa ya kufanya mazoezi Uwanja wa Mkapa siku moja kabla ya mchezo.

Wakati hayo yakitokea Bodi ya Ligi Kuu Tanzania Bara taarifa rasmi kupitia ukurasa wa Instagram imeeleza namna hii: “Ile siku imefika.” Taarifa hiyo imesindikizwa na ujumbe wa mechi ya Kariakoo Dabi ambayo inatarajiwa kufanyika Uwanja wa Mkapa.

Taarifa zinaeleza kuwa uongozi wa Simba haupo tayari kwa mchezo wa leo na wamegomea mazima suala hilo kwa mujibu wa kanuni.

KWA YANGA MECHI IPO PALE PALE

Iliwahi kutokea Mei 8 2021 ambapo uongozi wa Yanga uligomea mechi ya Dabi kwa kueleza kuwa mabadiliko ya muda yalifanyika kinyume na utaratibu kwa mujibu wa kanuni namba 15 ambayo ilikuwa inaeleza kuwa mabadiliko yoyote ya muda wa kuanza mchezo yatajulishwa ipasavyo kwa pande zote husika za mchezo angalau saa 24 kabla ya muda wa awali.

Katika siku hiyo Yanga walipeleka timu muda wa awali saa 11:00 jioni badala ya saa 1:00 usiku muda ambao Simba walipeleka timu. Mwisho mchezo huo ulipangiwa siku nyingine ambapo Yanga ilipata ushindi kwa bao 1-0 lililofungwa na Zawad Mauya.

Taarifa zinaeleza kuwa Yanga wao wapo tayari kwa mchezo na watapeleka timu kama ilivyo kawaida na hawana kipengele isipokuwa Simba wao wamegomea.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.