Milan wanaendelea kutafuta mshambuliaji mpya na mgombea wa hivi karibuni pamoja na Alvaro Morata ni mchezaji wa kimataifa wa Ujerumani Niclas Füllkrug.

Vyanzo vingi vina uhakika kwamba dili hilo limekamilika kwa Morata, ambaye ana kipengele cha kuachiliwa katika mkataba wake na Atletico Madrid na alikubali masharti binafsi.
Anaweza kufanyiwa vipimo vyake wiki ijayo, baada ya Fainali ya EURO 2024 kesho wakati Uhispania itamenyana na England huko Berlin.
Lakini, Milan pia wanataka mshambuliaji mwingine kuziba shimo lililoachwa na Olivier Giroud kwenda LAFC, wakihisi kwamba Luka Jovic hatatosha.

Pia meridianbet inatoa michezo ya kasino ya mtandaoni kama vile, Aviator, poker, Roullette, sloti na mingine kibao. Ingia meridianbet na ucheze sasa.
Tammy Abraham alitajwa kuhamia Milan kutoka Roma, lakini ni ghali kwa €25m na ana rekodi mbaya ya majeraha.
Sky Sport Italia inapendekeza mbadala wa kuvutia zaidi katika mchezaji wa kimataifa wa Ujerumani Füllkrug, ambaye akiwa na umri wa miaka 31 anaweza kuwa tayari kuondoka Borussia Dortmund.


