Mohamed Salah alithibitisha thamani yake kwa Liverpool tena alipoiongoza timu kushinda 5-0 dhidi ya West Ham na kuzidi kukaa kileleni kwenye msimamo wa EPL.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 32 alifunga goli lake la 20 msimu huu katika mashindano yote, akiwa mchezaji wa kwanza wa Reds kufikia alama hiyo kwa misimu nane mfululizo.
Pia Mohamed Salah alitoa pasi mbili za mabao, ya kwanza ikiwa ni ya kipekee ya goli la Cody Gakpo na ya pili kumuwezesha Diogo Jota kufunga goli la tano, yote hayo ikiwa ni siku tatu tu kabla ya kuwa huru kuanza kujadiliana na vilabu vya nje kuhusu uwezekano wa kuhamia msimu wa joto.
Trent Alexander Arnold, mchezaji mwingine muhimu kati ya watatu watakao maliza mikataba yao mwishoni mwa msimu pamoja na nahodha Virgil van Dijk, alifunga goli la nne, yote baada ya Luis Diaz kuanzisha uongozi kwa Liverpool waliokuwa wakitawala.
Ushindi mwingine mkubwa kwa timu ya Arne Slot, dhidi ya West Ham waliokuwa wanategemewa kushindwa, uliwaacha Liverpool wakiwa na pointi nane mbele kileleni mwa msimamo na hatua nyingine kuelekea kutwaa taji lao la kwanza kwa miaka mitano.
Hata hivyo, nafasi ya kwanza ya mchezo ilitengenezwa na wenyeji ambapo Jarrod Bowen alituma pasi nzuri kwa Lucas Paqueta, lakini mchezaji huyo wa Brazil aliteleza alipojaribu kupiga shuti na kupiga mpira juu na pembeni.
West Ham walijaribu kurejea kwa muda mfupi na walikuwa na bahati mbaya kutofunga wakati shuti la Mohammed Kudus kutoka umbali wa yadi 20 likipiga nguzo.
Mohamed Salah ambaye hakuwa na kifani alifanya ushirikiano wake wa 30 wa msimu, akichukua mpira kutoka nusu yake mwenyewe, akitembea mbele na kupiga pasi kwa Jota aliyetolewa benchi, ambaye alifunga goli la tano na kumaliza mwaka 2024 kwa mtindo kwa Liverpool.
Mechi inayofuata ya ligi, Liverpool atakuwa nyumbani kukiwasha dhidi ya Manchester united ya Amorim ambao wamekuwa na msimu mbaya.