Ismael Bennacer anadhani kwamba Milan iliweza kudhibiti hisia zao vizuri katika sare ngumu ya 1-1 dhidi ya Roma kwenye San Siro, akisema kuwa wangeweza pia ‘kuruhusu’ goli katika kipindi cha pili ambapo Giallorossi waliumba nafasi hatari.

Kiungo huyo wa Algeria alirejea uwanjani baada ya miezi minne ya jeraha kubwa na alikuwa na furaha kurudi, alipochukua nafasi ya Filippo Terracciano kipindi cha pili na kucheza dakika 45 zilizobaki.
Bennacer alisema kuwa, “Milan ilidhibiti hisia zao vizuri dhidi ya Roma lakini ilipoteza muendelezo. Nina furaha sana kurudi uwanjani, ilikuwa muhimu kwangu kwa sababu nilifanya kazi kwa bidii sana. Bennacer aliwaambia waandishi wa habari katika mkutano wa baada ya mechi. Sio rahisi kamwe kupona kutokana na majeraha kama haya.”
Pia meridianbet inatoa michezo ya kasino ya mtandaoni kama vile, Aviator, poker, Roullette, sloti na mingine kibao. Ingia meridianbet na ucheze sasa.
Mchezaji huyo aliendelea kusema kuwa ilikuwa mechi maalum kidogo kwake, hawakupoteza umakini na walidhibiti hisia zao vizuri. Wanaweza kuwa wameongoza, lakini pia wanaweza kuwa wameruhusu goli, mwishowe, hawakupoteza hivyo lazima waangalie mbele kwa sababu kuna lengo muhimu la kujiandaa nalo katika siku zijazo.



