Sergej Milinkovic-Savic : Bado nipo sana Lazio, Siendi Popote!

 

Kiungo wa klabu ya Lazio, Sergej Milinkovic-Savic amekanusha taarifa mbalimbali zinazomuhusisha na kuondoka ndani ya klabu hiyo katika majira ya baridi.

 

Taarifa zilizotoka hivi karibuni zilimuhusisha kiungo huyo kuondoka katika dirisha la usajili mwezi januari kutokana na kukosana na meneja wa klabu hiyo, Maurizio Sarri katika chakula cha usiku cha Christmass.

Manchester United ni moja ya klabu iliyokuwa inamfwatilia Milinkovic-Savic kwa muda mrefu na sasa wamehusishwa naye wakati kiungo Paul pogba kuhusishwa kuondoka mwishoni mwa msimu baada ya kugoma kuongeza mkataba ndani ya klabu hiyo.

Milinkovic-Savic alikanusha taarifa hizo katika akaunti yake ya Instagram :”Naona taarifa nyingi kuhusu mimi lakini… Sijali! Ninachotaka ni Lazio kushinda.”

Meneja, Maurizio Sarri pia alikanusha kuhusu kutofautiana na mchezaji huyo.

“Niligombana mara moja na Luis Alberto, miezi minne iliyopita.” alisema.

“Nimesoma moja kati ya habari kubwa ya uongo, kwamba nimegombana na Milinkovic-Savic. Sidhani.”


KUWA BINGWA MSIMU HUU WA SIKUKUU NA OCEAN CALL

Nani hapendi kuwa bingwa na kujishindia mkwanja wa kusahato kuelekea katika sikukuu wiki hii. Mchezo wa Ocean Call kutoka kasino maridhawa za meridianbettz unakupa kila sababu ya kuifanya siku kuu yako kuwa ya kuvutia zaidi.

tetesi, Tetesi za Soka Barani Ulaya., Meridianbet

CHEZA HAPA

Acha ujumbe