Mechi ya kwanza ya mapema hii leo baada ya Ligi kurejea itakuwa ni ya vijana wa Antonio Conte Tottenham Spurs watakuwa ugenini kuzichapa dhidi ya Brentford saa 9:30 mchana.

Spurs wamekuwa na msimu mzuri kutokana na matokeo wanayoyapata kwenye Ligi ambapo mpaka sasa wamejikusanyia pointi 29 kwenye michezo 15 waliyocheza wakiwa wamepoteza michezo minne pekee.
Brentford ya Thomas Frank wapo nafasi ya 10, wakiwa wameshinda mechi nne pekee, akaenda sare mara saba na akipoteza michezo minne, na pointi zake 19 kibindoni mpaka sasa.

Mechi ya mwisho nyuki walimfunga Bingwa mtetezi wa Ligi, City huku Conte na vijana wake nao wakiwachakaza Leeds United.
Ushindi utamfanya Spurs apande hadi nafasi ya 3 kwenye msimamo, wakati Brentford wao watapanda hadi nafasi ya 7.


